• Login
    View Item 
    •   MUT Research Archive
    • Journal Articles
    • School of Humanities and Social Sciences (JA)
    • Journal Articles (HSS)
    • View Item
    •   MUT Research Archive
    • Journal Articles
    • School of Humanities and Social Sciences (JA)
    • Journal Articles (HSS)
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    UWINGI-TAALUMA WA BEMBELEZI ZA WASWAHILI

    Thumbnail
    View/Open
    UWINGI-TAALUMA WA BEMBELEZI ZA WASWAHILI.pdf (632.6Kb)
    Date
    2025
    Author
    Akaka, Lina
    Maithya, Jane
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Dhana ya uwingi-taaluma ina maana ya kuunganisha au kuhusisha ujuzi anuwai wa kitaaluma katika mtazamo wa mada au tatizo. Mkabala wa uwingi-taaluma hulenga kueleza tatizo nje ya mipaka ya kawaida kwa kuungwa mkono na mikabala tofauti kutoka taaluma mbalimbali na kufikia suluhu zilizo na misingi yake katika uelewa wa hali changamano (Koski na Savolainen, 2016). Bembelezi za Waswahili zinaakisi uchangamano huo; kwamba zinaonekana kuwa na majukumu anuwai katika jamii. Majukumu kama vile ya utakasaji hisia, mawasiliano, uelimishaji halikadhalika uadilishaji. Majukumu haya ndio yanayoibua hisia kwamba zina uwingi-taaluma na hivyo kuwavutia watafiti kuchunguza taaluma mbalimbali zilizomo. Utafiti uliongozwa na nadharia ya uwingi-taaluma kwa mujibu wa Al-Saleem (2018). Data za bembelezi za Waswahili zilikusanywa katika Kisiwa Faza. Washiriki 11 wa kike wenye umri kati ya miaka 18 na 65 waliteuliwa kwa kuelekezwa na mmoja akateuliwa kimaksudi ili kusailiwa. Vikundi lengwa viwili vya mjadala, kila kimoja kikiwa na wasailiwa sita viliundwa kwa misingi ya umri, na data ya bembelezi 20 ikakusanywa kutokana na vikundi hivyo. Hatimaye bembelezi 10 ziliteuliwa kimaksudi ili kuchunguza uwingi taaluma uliomo. Data zilichanganuliwa kimaelezo. Matokeo ya utafiti yalionyesha dhahiri kwamba bembelezi zina uwingi-taaluma na hutumiwa katika miktadha ya shule, nyumbani, matibabu na mingineyo. Utafiti huu unatoa mchango wa kiusomi kwa watafiti wajao wa fasihi simulizi, wataalamu wa masuala ya elimu, wahudumu wa afya, wanasaikolojia na wanataaluma wengineo hususan wa taaluma zilizoshughulikiwa katika makala haya.
    URI
    https://doi.org/10.51317/eajk.v4i1.737
    http://repository.mut.ac.ke:8080/xmlui/handle/123456789/6555
    Collections
    • Journal Articles (HSS) [49]

    MUT Library copyright © 2017-2024  MUT Library Website
    Contact Us | Send Feedback
     

     

    Browse

    All of Research ArchiveCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    MUT Library copyright © 2017-2024  MUT Library Website
    Contact Us | Send Feedback